Wafanyabiashara wengi huanza biashara kwa nguvu, lakini bila mfumo rasmi wa hesabu za biashara. Mwanzoni inaweza kuonekana rahisi – kuandika mauzo kwenye daftari au kukariri kichwani. Lakini kadri biashara inavyokua, kutokuwa na mfumo wa mahesabu huanza kuleta hasara.
Mfumo wa hesabu za biashara sio kwa makampuni makubwa pekee. Ni kwa kila mfanyabiashara mdogo anayehitaji udhibiti wa fedha na faida.
Katika makala hii, utajifunza jinsi ya kuanzisha mfumo wa hesabu kuanzia sifuri.
Hatua ya 1: Tenganisha Fedha za Biashara na Fedha Binafsi
Hii ndio msingi.
Usichanganye:
- Mauzo ya biashara
- Pesa ya matumizi ya nyumbani
Fungua:
- Akaunti ya biashara (ikiwa inawezekana)
AU - Bahasha/box tofauti kwa pesa za biashara
Bila hatua hii, huwezi kujua faida halisi.
Hatua ya 2: Anzisha Mfumo wa Kurekodi Mauzo
Chagua mfumo rahisi lakini thabiti:
- Daftari la mauzo
- Excel
- Mfumo wa kidijitali
Rekodi:
- Tarehe
- Bidhaa
- Bei
- Kiasi
- Jumla
Rekodi kila siku. Usisubiri mwisho wa wiki.
Hatua ya 3: Rekodi Matumizi Yote
Wafanyabiashara wengi huandika mauzo tu.
Lakini faida hupatikana baada ya kutoa matumizi.
Rekodi:
- Gharama za manunuzi ya stock
- Kodi
- Umeme
- Usafiri
- Mishahara
Hata matumizi madogo ni muhimu.
Hatua ya 4: Fanya Hesabu ya Faida Kila Wiki au Mwezi
Faida = Mapato – Matumizi
Bila kufanya hesabu hii mara kwa mara, unaweza kudhani unapata faida wakati unapoteza.
Hitimisho
Kuanzisha mfumo wa hesabu za biashara sio jambo gumu. Kinachohitajika ni nidhamu.
Ikiwa unataka mfumo kamili, wa kitaalamu na unaoeleweka hatua kwa hatua, jiunge na Kozi ya Hesabu za Biashara na Usimamizi wa Kitaalamu ili ujifunze mfumo wa advanced unaokuwezesha kudhibiti fedha, stock na faida kwa uhakika.

