Kozi hii inakufundisha mifumo halisi ya hesabu za biashara zinazotumiwa na biashara imara kama kuhesabu COGS, gross profit, net profit, kuweka bei kwa asilimia sahihi, kusimamia stock, na kujenga rekodi za biashara zinazolinda faida.
Wajasiriamali wengi hufanya kazi kwa bidii lakini hawajui biashara yao inaingiza kiasi gani kweli. Kozi hii inabadilisha hilo. Utajifunza kuona biashara yako kwa data, kufanya maamuzi kwa hesabu, na kujenga mfumo wa fedha unaodumu.
Kupitia masomo ya wiki 6, utapata zana za vitendo, worksheet za biashara, na mifumo inayoweza kutumika mara moja. Lengo si nadharia — lengo ni kukupa uwezo wa kusimamia biashara yako kama taasisi.
Kozi hii inafaa kwa wamiliki wa biashara ndogo na za kati na kubwa wa Tanzania na Afrika Mashariki wanaotaka kukua kwa nidhamu, uwazi wa fedha, na faida halisi.
👉 Hii si kozi ya kubahatisha. Hii ni kozi ya wafanyabiashara wanaotaka udhibiti kamili wa mahesabu ya biashara zao.
